Psalms 18:2-7
2 a Bwana ni mwamba wangu,
ngome yangu na mwokozi wangu,
Mungu wangu ni mwamba,
ambaye kwake ninakimbilia.
Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu,
ngome yangu.
3 bNinamwita Bwana anayestahili kusifiwa,
nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 cKamba za mauti zilinizunguka,
mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
5 dKamba za kuzimu zilinizunguka,
mitego ya mauti ilinikabili.
6 eKatika shida yangu nalimwita Bwana,
nilimlilia Mungu wangu anisaidie.
Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu,
kilio changu kikafika mbele zake,
masikioni mwake.
7 fDunia ilitetemeka na kutikisika,
misingi ya milima ikatikisika,
vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Copyright information for
SwhKC